Proverbs 23:29-34


29 aNi nani mwenye ole?
Ni nani mwenye huzuni?
Ni nani mwenye ugomvi?
Ni nani mwenye malalamiko?
Ni nani aliye na majeraha yasiyo na sababu?
Ni nani mwenye macho mekundu?

30 bNi hao wakaao sana kwenye mvinyo,
hao waendao kuonja mabakuli ya mvinyo uliochanganywa.

31 Usiukodolee macho mvinyo wakati ukiwa mwekundu,
wakati unapometameta kwenye bilauri,
wakati ushukapo taratibu!

32 Mwishowe huuma kama nyoka
na kutia sumu yake kama nyoka mwenye sumu.

33 Macho yako yataona mambo mageni
na moyo wako kuwazia mambo yaliyopotoka.

34 Utakuwa kama alalaye katikati ya bahari,
alalaye juu ya kamba ya merikebu.
Copyright information for SwhKC